• SAFE & SECURE
  • Jina la Kitabu: MAJIBU KWA MASHAKA YAKO

    Mada kuu: Mambo ya Kiroho

    Upatikanaji:

    Utangulizi: Maswali muhimu ambayo hata wewe utaona jinsi yalivyo kana kwamba yanatokana nawe binafsi, ndiyo yanayojenga msingi kwa ajili ya majibu yanayohitajika. Kitabu hiki chenye kurasa 244 ambacho kimeandaliwa kwa namna hiyo ya maswali na majibu, kinajibu maswali kama vile Mungu ni nani? Uasi ulianzaje? Unabii unatuonesha nini? Wokovu ni nini? Hekalu ni nini? Tuko wapi katika ratiba ya ulimwengu? Biblia inasema nini juu ya tumbaku na vileo? Unawezaje kuwa na hakika ya kuingia mbinguni? Ondoa mashaka kwa kusoma kitabu hiki!
    TSH. 17,000
    Kiasi

    Jina la Kitabu: SABATO YA KWELI

    Mada kuu: Mambo ya Kiroho

    Upatikanaji:

    Utangulizi: “Je, ni Ijumaa, Jumamosi au Jumapili?” Hilo swali linajibiwa kwa utaratibu mzuri kutoka katika Biblia, mwongozo ukiwa hiki kitabu kidogo chenye kurasa 71. Mchungaji W. Duncan Eva anaeleza kwa ufupi juu ya undani wa Sabato ya kweli, ilipoanzia, uhusiano wake na Muumbaji, Kristo mwenyewe alivyosisitiza juu ya Sabato isivyobadilika, uhusiano wa mitume na Sabato, maana ya alama ya mnyama na mpango wa Mungu unavyodhihirika kupitia katika ukweli juu ya Sabato. Kitabu hiki pia kinasaidia kuona ni siku ipi leo ambayo ndiyo Sabato ya kweli na kisha kuwepo Sabato baada ya maisha ya dunia hii.
    TSH. 3,500
    Kiasi

    Jina la Kitabu: MISINGI YA NDOA

    Mada kuu: Ndoa

    Upatikanaji:

    Utangulizi: Joeli Chamba Matara, katika kitabu hiki anashughulikia mashaka kwamba ndoa zote huwa zina migogoro mfululizo maisha yote. Kwa sababu hiyo, ni kitabu hiki chenye kurasa karibia 70, ambapo huyu mwanandoa wa zaidi ya miaka 30 anaelezea misingi ambayo ikifuatwa, ndoa itadumu kwa furaha. Kusoma kitabu hiki kutakuwa ni hatua moja ya maana sana kujenga ndoa itakayodumu katika furaha.
    TSH. 8,300
    Kiasi
    View More Packages


    Copyright © 2018 - 2024. All Rights Reserved | HHESMS